3.2 KISWAHILI (102) 3.2.1 Kiswahili Paper 1 (102/1) 1 Lazima: Wewe ni

3.2 KISWAHILI (102)

3.2.1 Kiswahili Paper 1 (102/1)

1 Lazima:

Wewe ni meneja katika kampuni ya Jitihada ambapo pamekuwa na visa vya ukiukaji wa

maadili ya kikazi. Waandikie wafanyakazi memo kuwaonya dhidi ya jambo hili.

2 “Rununu (simutamba) imeleta athari mbaya katika jamii.” Jadili.

3 Andika kisa kitakachodhihirisha maana ya methali: Usitukane wakunga na uzazi ungalipo.

4 Tunga kisa kinachoanza kwa maneno yafuatayo:

Moyo wangu ulidunda kwa matarajio makuu …

11

3.2.2 Kiswahili Paper 2 (102/2)

1 UFAHAMU: (Alama 15)

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali.

Gari lake kuukuu lilikuwa linapambana na barabara yenye mashimo yaliyoshiba na kutapika

maji ya mvua ambayo sasa ilikuwa inaanza kupusa. Japo daima alipambana na usukani kunako

mashimo haya yaliyotosha kuitwa magenge, alishukuru kwa hali hii. Vipi angeweza kulidhibiti

gari lake hili kwenye barabara iliyosakafiwa nayo ikahitimu? Magurudumu haya yaliyong’ara

kama upara wa shaibu aliyekula chumvi hadi ikamwogopa yangetii uelekezi wake? Mara ngapi

gari hili limetaka kumwasi barabarani? Haya yalikuwa baadhi ya maswali yaliyompitikia akilini.

Hakujitakilifu kutaka kuyapa mji maana mara ile mawazo yake yalitekwa na kubwagwa katika

nchi ya mbali – nchi ambayo sasa aliiona kama sinema akilini mwake.

Alipofika  nyumbani  aliliegesha  gari  lake  na  kufululiza  ndani.  Siku  mbili  zilikuwa  zimepita

akiwa pale kazini. Madaktari kama yeye hawakuwa wengi. Alikuwa miongoni mwa madaktari

wenye ujuzi katika hospitali hii ya kitaifa. Wenzake wengi walikuwa wamehamia ughaibuni

walikokwenda kutafuta maisha. Mshahara wao wa mkia wa mbuzi uliwasukuma na kuwatema

nje ya nchi yao. Wengi wa waliohamia ng’ambo waliona vigumu kubaki katika ajira ambayo

kivuno chake kilishindwa kumvusha mtu hata nusu ya kwanza ya mwezi. Malalamishi ya kulilia

ujira wa heshima yaligonga kwenye masikio yaliyotiwa zege. Na kweli wanavyosema, mwenye

macho haambiwi tazama. Basi walitazama hapa na pale wakaona penye mianya ya matumaini,

nao wakaiandama.

Hadi leo hii hamna la mno lililofanyika. Ndiyo maana Daktari Tabibu anarudi nyumbani tangu

kuingia kazini hiyo juzi alfajiri. Hafanyi kwa kuwa katosheka, maana pia yeye ana dukuduku.

Ana shaka ya mustakabali wake ikiwa mazingira ni haya ya kumsoza, maana umri nao unazidi

kumla. Japo anatia na kutoa, mizani ya hesabu yake imeasi ulinganifu.

Daktari Tabibu waama ni mfungwa. Ametekwa na kuzuiwa katika kupenda na kuchukia mambo.

Ni kama mti uliodumaa. Anatamani barabara nzuri za lami. Anatamani mshahara wa kumwezesha

kukidhi mahitaji yake na kutimiza majukumu yake ya kimsingi.  Jana amesema na rafiki yake

aliye ng’ambo kwa simu ambayo sasa imetulia mkabala naye. Ingawa mwenzake huyu alikuwa

mchangamfu na kumdokolea hali ya maisha ya kuridhisha kule ugenini kama vile wanataaluma

kuenziwa, yapo vilevile yaliyomtia unyonge moyoni. Upweke ndio uliomtia fukuto kuu.  Licha

ya hela zote hizo za kupigiwa mfano, watu hawana muda wa kutembeleana na kujuliana hali

au hata kukutana tu mkahawani wakashiriki mlo. Eti ni kila mtu na hamsini zake. Halafu ipo

changamoto ya hali ya hewa. Baridi ya ng’ambo haifanyi mzaha katika kumtafuna mtu. Ni hali

tofauti na ile aliyoizoea.

12

Daktari Tabibu alizitia kauli za rafiki yake kwenye mizani ya moyo wake.   Akawaza ikiwa

kweli si bora kulemazwa na mzizimo ugenini badala ya kuishi katika kinamasi cha kuumbuliwa

nyumbani. Kisha punde lilimjia wazo la marehemu nyanyake na wengine kama yeye waliofadhili

masomo yake kupitia kwa serikali na njia ya kodi. Je, si usaliti huu? Vipi aikimbie nchi kabla

ya kuihudumia ilhali imemjenga hadi kuwa daktari? Na je, wafanyakazi wake wa nyumbani

watakwenda wapi?Atawaambiaje kuwa sasa hahitaji huduma zao kwa kuwa anakimbia nchi

yake?

Mawazo yake yalikatizwa na simu iliyolia na kumshtua. Alipoitazama aliiona imeng’ara kwa

mwangaza ulioweka wazi jina la mpigaji. Alifahamu kuwa leo hii tena dharura nyingine ilikuwa

inamwalika hospitalini. Mwili wake ulimsaliti ingawa moyo wake ulimkumbusha kuwa lisilo

budi hutendwa. Hapo ndipo alipoiinua ile simu tayari kusema na mwenzake upande wa pili.

“Haloo!” Sauti nyororo kutoka upande wa pili iliita.

“Haloo!”

“Naam! Dharura nyingine tena daktari. Unaombwa kuokoa maisha mengine tena!”

“Haya. Ila mwanzo nitahitaji kujimwagia maji”, na pale pale akaikata ile simu.

Daktari Tabibu aliingia hamamuni huku kajifunga taulo kiunoni tayari kuoga. Aliyafungulia maji

lakini ule mfereji uligoma kutapika maji. Ulikuwa umekauka kabisa. Daktari Tabibu aliduwaa

pale. Aliufunga ule mfereji kabla ya kuiaga bafu.

(a) Eleza sababu nne zinazowafanya wataalamu kuhamia nchi za nje. (alama 4)

(b) “Hakuna masika yasiyokuwa na mbu.” Thibitisha kauli hii kwa kurejelea hali ya

waliohamia ng’ambo. (alama 3)

(c) Fafanua athari tatu zinazoikumba nchi ya msimulizi kutokana na uhamiaji ng’ambo wa

wataalamu. (alama 3)

(d) Eleza mchango wa teknolojia kwa kurejelea kifungu. (alama 3)

(e) Eleza maana za msamiati ufuatao kulingana na taarifa. (alama 2)

(i) kuyapa mji

(ii) fukuto

13

2 UFUPISHO: (Alama 15)

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali.

Wakenya  walipoipitisha  katiba  mpya  waliidhinisha  mfumo  wa  ugatuzi.  Katika  mfumo  huu,

mamlaka ya serikali kuu katika uongozi, usimamizi na utumiaji wa rasilimali za nchi hupunguzwa.

Kiasi fulani cha mamlaka hutwaliwa na maeneo ya ugatuzi. Suala hili halikuzingatiwa katika

katiba ya awali ambapo mamlaka yote yalikuwa mikononi mwa serikali kuu. Kutokana na upana

na wingi wa maeneo nchini, iliiwia vigumu serikali kuu kuhakikisha kwamba kulikuwa na usawa

wa kimaendeleo katika sehemu zote nchini.

Kwa mujibu wa katiba mpya, serikali kuu haina budi kuyasaidia maeneo yote ya ugatuzi ili

yaweze kujinyanyua kiuchumi na kuboresha hali za maisha za wakazi wake. Vilevile ni jukumu

la kila eneo la ugatuzi kuweka mikakati madhubuti ili kuchunguza na kubainisha rasilimali zote

katika maeneo husika. Hili litasaidia kuvumbua rasilimali ambazo zinaweza kuchangia katika

ustawishaji wa maeneo haya. Maeneo haya pia yanatakiwa kutafuta mbinu zitakazofanikisha

uzalishaji na utumiaji wa rasilimali hizi kwa njia endelevu. Mojawapo ya mbinu hizi ni uongezaji

thamani katika rasilimali yoyote inayozalishwa kwenye eneo mahususi.

Maeneo mengi ya ugatuzi nchini humu yanategemea kilimo cha ufugaji kama mhimili wa uchumi.

Licha ya kuwa nguzo, kilimo hiki hakijawahi kupigiwa darubini vizuri kwa lengo la kukiimarisha

ili kiwanufaishe wenyeji kikamilifu. Aghalabu wafugaji wengi huandama mbinu za jadi za ufugaji

ambazo haziwahakikishii ongezeko la mapato. Isitoshe, wafugaji hawa wanakabiliwa na tatizo

katika soko la mifugo ambapo wengi hupunjwa na matapeli. Pamoja na haya, baadhi ya wakazi

huuza mifugo nje ya nchi wakiwa wazimawazima bila kuwazia matokeo ya kitendo hiki.   Si

ajabu kuwaona ng’ombe, ngamia, mbuzi na kondoo wakipakiwa kwenye malori na kusafirishwa

nje ya nchi. Ukweli ni kwamba jambo hili ni hatari sana, si kwa uchumi wa maeneo husika tu,

bali pia kwa Kenya kwa jumla. Hii ni kwa kuwa walionunua mifugo wazimawazima wanaweza

kuhiari kutowachinja na badala yake kuwatumia kama mbegu za kuzalisha mifugo wao. Hapa

pana  hatari  ya  maeneo  haya  kupoteza  wateja  kwani  baada  ya  muda  huenda  wanaonunua

mifugo wakajitosheleza na kukosa kuja kununua mifugo wengine. Hali ikiwa hivyo, maeneo

yaliyotegemea soko hili huenda yakalipoteza taratibu, na bila shaka kupoteza natija inayotokana

na soko lenyewe.

Ili  kudhibiti  hali  hii,  itakuwa  bora  ikiwa  viwanda  vya  kuchinjia  mifugo  na  kupakia  nyama

vitajengwa katika maeneo haya ya ugatuzi. Hili litawawezesha wakazi kuuza nyama badala ya

kuuza mifugo wazimawazima. Fauka ya haya, maeneo haya yatajikinga dhidi ya kupoteza bidhaa

zinazotokana na mifugo.   Hizi ni kama vile ngozi, kwato na pembe ambazo bila shaka zina

14

natija kuu. Ngozi kwa mfano, ni bidhaa muhimu sana katika sekta ya utengenezaji wa mavazi na

mifuko. Viwanda vinavyotumia ngozi kama malighafi vikijengwa katika maeneo haya, wakazi

wake watanufaika si haba. Mathalani, viwanda vya kutengenezea viatu, mishipi, mifuko na nguo

vikianzishwa, wawekezaji watalazimika kuanzisha viwanda vingine vitegemezi. Kadhalika, ni

dhahiri kwamba bidhaa zinazotokana na ngozi huhitaji kutiwa nakshi. Kuanzishwa kwa viwanda

hivi basi kutazua haja ya kuanzishwa kwa viwanda vya kutengenezea rangi, pamoja na maduka ya

kuuza bidhaa yenyewe. Isitoshe, gundi ya kugandisha bidhaa hizi itahitajika, hivyo kusababisha

haja ya kuanzishwa kwa kiwanda cha gundi. Matokeo ya shughuli hizi zote ni kuzalishwa kwa

nafasi anuwai za kazi kwa wakazi. Hili litakuwa na matokeo zaidi chanya, hususan kwa vijana.

Badala  ya  kushiriki  ulevi  na  burudani  zinazowahatarisha,  wataweza  kujitafutia  riziki  katika

viwanda hivi.

Juu ya hayo, mfumo wa ugatuzi utayawezesha maeneo husika kuongezea thamani utoaji wa

huduma za kijamii na kiutawala kulingana na mahitaji ya maeneo haya. Ni muhimu hata hivyo

kuzingatia  kwamba  kila  eneo  la  ugatuzi  lina  upekee  wake,  navyo  vipaumbele  hutofautiana

kulingana na maeneo. Kuna yale ambayo yatasisitiza usalama, mengine ujenzi na uimarishaji wa

miundomsingi kama vile barabara, vituo vya afya na hata taasisi za elimu. La muhimu ni wakazi

wa maeneo husika kubainisha ni lipi litatekelezwa kwanza.

Kinga na kinga ndipo moto uwakapo. Kufanikiwa kwa mfumo wa ugatuzi kutategemea juhudi za

kila mkazi wa eneo husika. Ni muhimu kila mkazi kujiona kuwa mmiliki wa eneo zima la ugatuzi

na kuwajibika katika kuliendeleza kwa hali na mali. Uwajibikaji huu unajumuisha uteuzi wa

viongozi wenye muono mzuri na ambao watawawezesha kuyafikia malengo yao ya kimaendeleo.

Hakika, mustakabali na uwepo wa eneo la ugatuzi utakuwa zao la maamuzi ya wanaeneo. Vilevile

ufanisi wa maeneo ya ugatuzi utakuwa msingi wa ufanisi wa taifa kwa jumla.

(a) Fupisha ujumbe wa aya tatu za mwanzo kwa maneno 85-90.

Matayarisho:

(alama 8, 1 ya mtiririko)

Nakala safi:

(b) Kwa kutumia maneno 75-80, bainisha masuala ambayo mwandishi anaibua katika

aya tatu za mwisho. (alama 7, 1 ya mtiririko)

15

3 MATUMIZI YA LUGHA: (Alama 40)

(a) (i) Eleza maana ya sauti mwambatano. (alama 2)

(ii) Andika sauti mwambatano inayotamkiwa kwenye ufizi. (alama 1)

(b) Andika sentensi ifuatayo upya ukibadilisha neno lililopigiwa mstari kuwa kielezi.

Komu ameshona nguo nzuri na kuiuza sokoni. (alama 1)

(c) Tunga sentensi mojamoja kubainisha: (alama 4)

(i) kihusishi cha wakati

(ii) kivumishi cha pekee chenye maana, “bila kubagua”.

(d) Andika sentensi ifuatayo katika hali yakinishi.

Askari wasipopiga doria wala kushirikiana na raia hawatakuwa wametuhakikishia

usalama. (alama 2)

(e) Bainisha mofimu katika neno:

atamnywea (alama 3)

(f) Andika sentensi ifuatayo katika hali ya udogo:

Madebe hayo yatasafirishwa pamoja na nyundo hizi. (alama 2)

(g) Ainisha vishazi katika sentensi ifuatayo:

Ingawa mshahara wake si mkubwa anaikimu familia yake. (alama 2)

(h) Tunga sentensi tatu kuonyesha matumizi matatu tofauti ya kiambishi ‘li’. (alama 3)

(i) (i) Eleza maana ya sentensi ya masharti. (alama 1)

(ii) Tunga sentensi ya masharti. (alama 2)

(j) Tumia kiwakilishi cha ‘a’ unganifu katika sentensi kuonyesha:

(i) umilikaji

(alama 2)

(ii) nafasi katika orodha au nafasi katika kundi (alama 2)

(k) Tunga sentensi yenye kikundi tenzi chenye muundo ufuatao:

Kitenzi kisaidizi, kitenzi kikuu, nomino (alama 2)

(l) Tunga sentensi mbili kuonyesha matumizi mawili tofauti ya kistari kirefu.

16

(alama 2)

(m) Unganisha sentensi zifuatazo kuwa sentensi moja bila kurudia kitenzi.

Osore amempigia Ngungui simu. Ngungui amempigia Osore simu. (alama 2)

(n) Andika upya sentensi ifuatayo ukibadilisha vitenzi vilivyomo kuwa nomino:

Mayaka anapotumbuiza huchekesha sana. (alama 2)

(o) Andika maana tatu za neno:  kanda. (alama 3)

(p) Andika visawe viwili vya nahau: enda kombo. (alama 2)

4 ISIMUJAMII: (Alama 10)

Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali.

Haya ng’ara …  Ng’ara leo! Nguo motomoto. Ng’ara leo kwa bei rahisi. Hamsini hamsini shati.

Kuona ni bure. Bure kwa bure. Shika mwenyewe ujionee. Bei nafuu. Bei ya starehe. Haya

haya. Usikose mwanangu! Hamsa! Fifty! Hamsa! Fifty! Hamsa na nyingine.

(a) Bainisha sajili ya mazungumzo haya. (alama 2)

(b) Eleza sifa nane za sajili hii kwa kurejelea kifungu hiki. (alama 8)

17

(c) Eleza mbinu sita unazoweza kutumia katika kukusanya na kuhifadhi habari

3.2.3 Kiswahili Paper 3 (102/3)

SEHEMU A :  FASIHI SIMULIZI

1 Lazima

(a) Huku ukitoa mfano, eleza maana ya vitanza ndimi. (alama 2)

(b) Fafanua majukumu sita ya vitanza ndimi katika jamii. (alama 6)

kuhusu vitanza ndimi. (alama 12)

SEHEMU B:  RIWAYA

Said A. Mohamed: Utengano

2 “Walifanya kazi, walimenyeka,

Njaa, ndiyo ilikuwa misumenoLakini walilala na njaa …

Iliyokeketa matumbo yao, …”

Jibu swali la 2 au la 3.

kauli hii. (alama 2)

(c) Kwa kurejelea tamthilia, fafanua mifano mingine saba ya matumizi ya tamathali(a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)

(b) Bainisha tamathali mbili za usemi zinazojitokeza katika dondoo hili. (alama 4)

(c) Kwa kurejelea riwaya, onyesha jinsi wanyonge walivyomenyeka. (alama 12)

3 Jadili uhusiano uliopo kati ya wahusika na maudhui kwa kurejelea wahusika wafuatao:

(a) Shoka (alama 10)

(b) Kazija (alama 10)

SEHEMU C: TAMTHILIA

T. Arege:  Mstahiki Meya

Jibu swali la 4 au la 5.

4 Jadili mchango wa Wanacheneo katika kuivunja jamii yao. (alama 20)

5 “Ndiyo hivyo bwana.  Elimu yetu hapa ni ya kawaida mno.  Haina kubwa la kumfaa mtoto

mwenye mzazi anayeona mbali.”

(a) Eleza muktadha wa maneno haya. (alama 4)

(b) Bainisha tamathali ya usemi inayojitokeza katika dondoo hili ukirejelea msemaji wa

uliyotaja katika (b) hapo juu. (alama 14)

18

Nikaiga rika langu, kwa vileo na mbio za wasichana,

Ni wakati utanena.

Wapitao wakiimba, eti mimi, ningapenda hali zao,

Eti ni kwa raha zao.

Ni mtu kuwa hawara, wa vitimbi, ama alozawa tasa?

Waama sina makosa.

Muwaite watribu, kina Siti, watuzwa ilimu hiyo,

Kwalo sichafuki moyo.

Siwi nikaona ghere, lailatu, nyota njema itafika,

Akiri amejibika.

SEHEMU D:   USHAIRI

Jibu swali la 6 au la 7.

6 Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.

Sinongi aushi yangu, hii leo, kwa ukungu wa ujana,

Kiwa ni riziki yangu, mapokeo, kuoa na kuona,

Nashukuru kwa ugumba, wenye ndimi, wanipagazao nao,

Haupandiki mgomba, wana nyemi, fisadi wa hadhi zao,

Ni lipi lenye kukera, kwa Muumbi, marufuku kwenye misa,

Ugumba na ukapera, sio dhambi, wala haujawa kosa,

Bora tungeni vitabu, magazeti, mutangaze kwa rediyo,

Na zaidi muhutubu, kwa umati, muwambe ambayo siyo,

Hidhuru yote ni bure, sio kitu, kudhiki asodhikika,

Kwa shangwe na njerejere kila mtu, mdomo utafumuka,

(Mwalaa M. Nyanje)

(a) Eleza jambo ambalo mzungumzaji (nafsineni) katika shairi hili anasingiziwa.

(alama 2)

(b) Fafanua mambo matano ambayo mzungumzaji (nafsineni) anapinga katika shairi hili.(alama 5)

(c) Eleza umuhimu wa viishio vya beti za shairi hili. (alama 2)

(d) Andika ubeti wa tatu kwa lugha ya nathari. (alama 4)

(e) Eleza muundo wa shairi hili. (alama 5)

(f) Bainisha matumizi mawili ya tasfida katika shairi hili. (alama 2)

19

7 Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.

1   Huno wakati mufti, vijana nawausia,

Msije juta laiti, mkamba sikuwambia,

Si hayati si mamati, vijana hino dunia,

Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula.

2   Japo aula kushufu, na machoni vyavutia,

Dunia wana dhaifu, yaugua nisikia,

Vijana nawasarifu, falau mkisikia,

Ukiona vyang’aria, tahadhari vitakula.

3   Jepusheni na zinaa, mlale penye sheria,

Msije andama baa, makaa kujipalia,

Jepusheni na zinaa, madhara kukadiria,

Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula.

4   Ngawa waone wazuri, nadhifu kukuvalia,

Wajimwaie uturi, na mapoda kumichia,

Si mlango nyumba nzuri, ngia ndani shuhudia,

Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula.

5   Wawapi leo madume, anasa walopapia?

Wamepita ja umeme, leo yao sitoria,

Shime enyi wana shime, bora kumcha Jalia,

Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula.

6   Nambie faida gani, nambie ipi fidia?

Upatayo hatimani, waja wakikufukia,

Ila kufa kama nyani, kasoro yako mkia,

Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula.

7   Kikiki ikaze kamba, u kijana vumilia,

Ujifanye kama kwamba, u jiwe huna hisia,

Wakwambe watalokwamba, kwa lolote vumilia,

Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula.

8   Vyatiririka tiriri, vina vyanikubalia,

Alo bora mshairi, pa tamu humalizia,

Nahitimisha shairi, dua ninawapigia,

Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula.

(b) Fafanua kwa kutoa mifano, mbinu nne alizotumia mshairi kutosheleza mahitaji ya

(c) Nafsineni (mzungumzaji) katika shairi hili inasema na pande mbili.  Zieleze pande hizo.

“Kikaza”   (Robert Oduori)

8 ‘Wakaacha chungu kinatokota – bila kuivisha chakula’.  Kwa hakika walijibu, “Ndio mtindo, na

kuivisha chakula. (alama 16)9.   Ewe Mola mtukuka, si shaka wanisikia,

Wakingie wanarika, na anasa za dunia,

Amina wangu Rabuka, dua yangu naishia,

Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula.

(Mwalaa M. Nyanje)

(a) Eleza ujumbe wa shairi hili. (alama 4)

kiarudhi katika shairi hili. (alama 8)

(alama 2)

(d) Eleza umuhimu wa maswali ya balagha katika shairi hili. (alama 3)

(e) Bainisha toni ya shairi hili. (alama 3)

SEHEMU E: HADITHI FUPI

K Walibora na S. A. Mohamed: Damu Nyeusi na Hadithi Nyingine

sisi tulifuata mitindo.”

(a) Fafanua muktadha wa dondoo hili. (alama 4)

(b) Onyesha jinsi Wanatekede wanavyofuata mitindo na kuacha chungu kinatokota bila

20

Visit www.kcse-online.info for thousands of revision materials

The post 3.2 KISWAHILI (102) 3.2.1 Kiswahili Paper 1 (102/1) 1 Lazima: Wewe ni appeared first on PapersSpot.

GET HELP WITH YOUR HOMEWORK PAPERS @ 25% OFF

For faster services, inquiry about  new assignments submission or  follow ups on your assignments please text us/call us on +1 (251) 265-5102

Write My Paper Button

WeCreativez WhatsApp Support
We are here to answer your questions. Ask us anything!
👋 Hi, how can I help?
Scroll to Top